Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imetoa mafunzo ya dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi kwa Kanisa katoliki na mashirika yake nchini zikiwemo shule, hospitali, vituo vya kulelea Watoto yatima, wagonjwa na huduma nyingine za kijamii.
Mafunzo hayo yalifunguliwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Padri Dkt. Charles Kitima.